Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Goodluck Ole-Medeye wakati akijibu
swali la nyongeza la Mbunge wa Kilindi Dastan Kitandula (CCM).
Ole Medeye alisema kuwa uamuzi wa kufuta hati miliki hizo kwa sasa uko mikononi mwa Rais baada ya kukamilika kwa hatua zote.
Katika swali hilo Kitandula alitaka kujua ni lini
Serikai itafuta hati miliki kwa mashamba ya mkonge ambayo kwa muda mrefu
yametelekezwa ili kuwagawia wananchi wenye uhitaji.
Awali, Herbert Mtangi (Muheza-CCM) alitaka kujua
ni viwango gani stahiki ambavyo wawekezaji wa zao la katani wanatakiwa
kulipa kama ushuru kwa halmashauri husika.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa Hawa Ghasia, alisema kuwa halmashauri zote
nchini zimepewa mamlaka ya kutoza ushuru wa mazao chini ya kifungu 7 (1)
(g) cha sheria ya fedha za serikali za Mitaa.
“Ushuru huu hulipwa na mununuzi na unatozwa mahali
ambapo zao linazalishwa na kwa bei ya mkulima yaani bei ya zao kabla ya
kuongezwa thamani,” alisema Ghasia.
Alisema wafanyabiashara wote wa zao la
mkonge,wanatakiwa kulipa ushuru wa mazao ambao ni kuanzia asilimia 3
hadi 5 kwa mujibu wa sheria.
Wakati huohuo, Naibu Waziri wa Maji, Dk Binilith
Mahenge amemtetea bosi wake, Profesa Jumanne Maghembe kuhusu tuhuma
zilizoelekezwa kwake za kupeleka mradi mkubwa wa maji jimboni kwake,
huku wilaya zingine zikiachwa ‘yatima’.
Akijibu hoja mbalimbali za wabunge jana, Dk Mahenge alisema mradi wa Mwanga-
Same-Korogwe ni mwendelezo wa miradi mikubwa ya maji kama ule wa Chalinze.
“Yote yaliyoelezwa tutayazingatia. Ni kweli
kutokana na unyeti wa suala la maji, lazima hisia zitapelekea mawazo
mengi juu ya kasungura kadogo kuonekana mtu mmoja amejimegea wengine
hakuna,” alisema Dk Mahenge.
No comments:
Post a Comment