Sunday, April 27, 2014

VIONGOZI WA CCM SENGEREMA WAVURUGANA

 Sengerema
Katibu wa chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza Bw Mohamed Shaaban Mohamed,  amekuwa na malumbano na viongozi  wa umoja wa vijana UVCCM  Bw Robert Madaha na Bw Benedicto Bujiku baada ya mwenyekiti wa umoja huo Bw Madaha kusema hatoshi katika nafasi yake ya ukatibu  kwa viongzi wa mkoa walipokuja kuhudhuria kwenye kikao cha kamati ya siasa wilaya sengerema kilichofanyika march 22, mwaka huu.
 
Wakiongea na mwandishi wa habari hizi  kwa nyakati tofauti viongozi hao wa  umoja wa vijana  walisema kuwa hawakuwahi kuwa na malumbano yoyote na katibu wa chama hicho Bw Mohamed isipokuwa malumbano yao yalianza march mwaka huu baada ya viongozi wa mkoa kuwasili sengerema march mwaka huu kwa lengo la kujadili watumishi wa chama katika mienendo yao ya kazi.
 
Aidha Madaha aliongeza kuwa baada ya kumaliza kikao baadhi ya wajumbe ambao sio waadilifu walivujisha siri na kumwambia Katibu wao kuwa hatoshi katika nafasi yake apelekwe mtu mwingine atakaeziba pengo lake ambapo tangu hapo Mohamed alianza ktafuta visa vya kumng’oa nafasi yake ili asiwe anahudhuria kamati ya siasa wilaya.
 
“Mimi Mohamed mambo yote anayoniundia ya vijana kunipiga mawe ni kwasababu tu walikuja katibu wa CCM Mkoa akiwa na baadhi ya viongozi wenzake kwenye kamati ya siasa ya mwezi wa tatu…… katika kujadili masuala ya watumishi baadhi walitoka nje ili tujadili na tukajadili vizuri na ilipofika zamu ya wengine nao walitoka wakajadiliwa ila sasa baada ya hapo kuna mwenzetu mmoja ambaye ni diwani mwenzangu sipendi kumtaja jina alimfuata katibu na kumwambia kuwa madaha amekuharibia kwa viongozi” alisema madaha.
 
Hata hivyo baada ya siku chache kupita inasadikiwa katibu wa CCM wilaya aliwahamasisha wajumbe na wasiokuwa wajumbe wa umoja wa vijana CCM  kwenda polisi kufungua kesi ya wizi wa pikipiki za umoja huo ambapo walifanikiwa kufika polisi na kufungua kesi ya wizi wa pikipiki na hadi sasa inaendelea.
 
Aidha upotevu wa pikipiki hizo pia kuna muhusisha katibu wake wa vijana ambapo baada ya kumuhoji katibu huo wa vijana kuhusiana na upotevu wa piki piki hizo alidai kuwa kweli pikipiki hizo waliziuza kwa watu watatu tofauti na bei tofauti kutokana na ubora wake na kuongeza kuwa waliziuza kisheria kwa kufuata utaratibu wa umoja wao, ambapo kamati nzima tendaji ilikaa kikao cha kuuza piki piki hizo na wajumbe waliohudhuria walisaini kitabu cha mahudhulio.
 
  Nashangaa kwanini Mohamedi ananing’ang’ania mimi wakati piki piki ziliuzwa tangu mwaka jana kabla hata hajaja alikuwepo Yule katibu mwingine Magdalena leo hii baada ya kukorofishana na madaha tu na mimi naingizwa katika mkumbo huo yeye alisema shida yake ni mwenyekiti wa vijana na sio mimi……. Ndugu mwandishi kinachogomba hapo ni mimi kuwa karibu na m/kiti wangu haaya yote ni majungu ya kisiasa tu hakuna ukweli wowote.” Alisema Bujiku.
 
Katibu wa chama hicho alipoulizwa kuhusu suala hilo alichojibu shida yake ni umwenyekiti wa umoja huo  na sio udiwani wa Madaha ambapo alisisitiza kuwa mwenyekiti huyo ajiuzuru wadhifa wake, na kuongeza kuwa ili Bujiku apone aachane na madaha na akiendelea kuwa nae pamoja ataharibikiwa.
 Na Dotto Mgaza

No comments: