Sunday, April 27, 2014

MKAKATI WA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA PALEST. WAANZA

Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina hivi karibuni ataanzisha mazungumzo na pande husika kwa minajili ya kuunda serikali ya umoja wa kitaifa huko Palestina. Taarifa zinasema kuwa, Mahmoud Abbas anakusudia kukutana na makundi na shakhsia mbalimbali huru ili kujadiliana nao kuhusu mchakato wa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa. Taarifa zinasema kuwa, Abbas atajadiliana na makundi na shakhsia hao kuhusiana na mawaziri watakaounda serikali ya umoja wa kitaifa, na kisha kuandaa mazingira ya kuitishwa uchaguzi wa rais na bunge. Duru za kisiasa zinaeleza kuwa, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ana mpango wa kuunda serikali itakayowashirikisha shakhsia huru na wasiofungamana na mirengo ya kisiasa, akihofia radiamali itakayotolewa na utawala wa Kizayuni wa Israel na Marekani. Inafaa kuashiria hapa kuwa, hivi karibuni harakati za Fat–h na Hamas zilitiliana saini makubaliano ya  kuundwa serikali ya umoja wa kitaifa katika kipindi cha wiki tano zijazo, ambayo itasaidia kuondoa mivutano na mifarakano kati ya pande hizo mbili.

No comments: