Monday, September 8, 2014

`Kujiuzulu mwanasheria wa Zanzibar hakutaathiri Bunge`

Bunge Maalum la Katiba limesema kujiuzulu kwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar katika Kamati ya Uandishi wa Katiba mpya hakutaathiri upatikanaji wa katiba mpya.

Katibu wa Bunge hilo, Yahya Khamis Hamadi, alisema kitendo cha kujiuzulu kwa mwanasheria mkuu, Othman Masoud Othman, ni jambo la kawaida na kwamba uwakilishi wa Zanzibar ndani ya chombo hicho utakuwepo.

Alisema hajapata taarifa rasmi ya kujiuzulu kwa Othman katika kamati hiyo ambayo ipo chini ya Uenyekiti wa Mbunge wa Bariadi Mashariki, Adrew Chenge, lakini kama amefanya hivyo atakuwa ametimiza wajibu wake kisheria.

Hamad, alisema kwamba mwanasheria huyo hakuingia katika Kamati ya uandishi wa Katiba mpya kutokana na wadhifa wake, bali ni uteuzi wake ulifanywa na uongozi wa Bunge hilo kama wajumbe wengine.

Katibu huyo aliongeza kuwa uwakilishi wa Zanzibar katika kamati hiyo utakuwepo kwa sababu kuna wajumbe wengine kutoka upande huo wa Muungano wanaendelea na kazi hiyo kikamilifu.
 

No comments: