Monday, September 8, 2014

DALADALA ZAGOMA KUTOA HUDUMA MANISPAA YA IRINGA

KITUO CHA MABASI MIYOMBONI KUKIWA HAKUNA DALADALA HATA MOJA BAADA YA KUGOMA

STENDI YA MASHINE TATU ABIRIA WAKISUBIRI DALADALA BAADA YA KUGOMA KUTOA HUDUMA
BAADHI YA ABIRIA WAKILAZIMIKA KUTUMIA USAFIRI WA TOYO BAADA YA DALADALA KUGOMA



MADEREVA wa daladala manispaa ya Iringa leo wameanza mgomo usio na kikomo” wakizishinikiza mamlaka zinazohusika kuwazuia madereva wa pikipiki za miguu mitatu Bajaj” kufanya biashara ya daladala. 
Hatua hiyo imeleta adha kubwa kwa watumiaji wa usafiri wa daladala japokuwa imekuwa neema kubwa kwa waendesha bodaboda, Bajaj na malori madogo aina ya Suzuki Carry. 
Wakizungumzia mgomo huo, baadhi ya wakazi wa mjini hapa wamesema kwamba umewaathiri kwa kiasi kikubwa huku wakiutupia lawama uongozi wa mamlaka ya usafiri wan chi kavu na majini (SUMATRA) mkoa wa Iringa.
Aidha mmoja wa madereva wa daladala hao ambaye hakutaja jina lake amesema kuwa tatizo hilo la mgomo ni kutokana na utaratibu mbovu wa waendesha bajaji.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha wasafirishaji kwa kutumia pikipiki mkoa wa Iringa Bw. Joseph Mwambabe, amewatupia lawama viongozi wa Sumatra kwa kuuchochea mgomo huo
Hata hivyo Mwambabe  amesema tatizo hilo wamelifikisha katika ofisi za mkuu wa mkoa na mpaka sasa wanasubiri unatatibu utakao waongoza katika kazi zao.
 Mgomo huo umechukua zaidi ya masaa 10 kuanzia saa kumi na mbili hadi habari hii inatumwa ulikuwa bado ukiendelea Mjengwablog lilimtafuta Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Leopord Fungu ofisini kwake alikuwa katika kikao pamoja viongozi wa kamati ya usalama barabarani kwa kushirikiana na uongozi wa Sumatra mkoa wa Iringa.

No comments: